Tuesday, December 29, 2009

Stools, Tshs. 100,000/- @ toa order sasa!!!!


ENJOY THE PHOTOS



HOME WITH FRIENDS & FAMILY ILIKUWA KABLA YA X-MASS
SO NAWATAKIA MWAKA MPYA NDUGU ZANGU, WOTE, WENYE HERI NA MAFANIKIO. NA WANABLOG, WAPENZI WASOMAJI WA BLOG YA SYLVIA
NA WATANZANIA WENZANGU POPOTE WALIPO MUNGU AWAJALIE KTK KILA JAMBO JOSSYANNE KOKU MWESIGA GEORGE.




DADA NA WENGINEO WOTE TUNAWATAKIA MWAKA WA MAFANIKIO, NA BARAKA
MI JOSSYANNE & SYLVIA.& HER CAMPANY , THANK YOU.

Monday, December 28, 2009

Nimerudi kutoka mapumziko ya sikukuuuu!!!

Habari za holiday.

Namshukuru mungu kila kitu kilikwenda sawa, na nilikuwa na familia na nilipata nafasi ya kupumzika.

Nawatakia kila la kheri kwenye matayarisho ya kuukaribisha mwaka mpya.

From
Sylvia

Wow, angalia ukuta!!!

Monday, December 21, 2009

MALI MPYA KWA X- MASS IKO DUKANI. NA KWA BEI ZA SIKUKUUUU. KARIBUNI

Karibuni dukani Kreative Homez(Homez Deco) mali mpya kwa ajili ya x-mass, mito ipo ya saizi zote na unatengenezewa foronya kutokana na unavyopenda na rangi unazozipenda, wa futi 6 ni tshs 60,000/= wa futi 7 ni tshs. 75,000/- ikiwa na mapambo na box za zawadi kama inavyoonekana. ikiwa bila mapambo wa futi 6 ni 30,000/- na wa futi 7 ni 37,000/=
tshs. 30,000/-
tshs. 30,000/-
Candle holder na candle ni ths 35,000/-
Hizi zinaitwa humper, kuna zenye wine, champaign, mishumaa, etc. na kama una zawadi ama vitu vya kuweka kwenye humper unahitaji tukufungie karibu dukani. kuna ya kuanzia 52,500 - 41,000/= .


mito ya saizi zote ipo. njooo utoe order na utupe rangi unazohitaji utatengenezewa. mikubwa kabisa 50,000/- midogo 10,000, saizi inayofuata 15,000/=, mto wa kitandani 20,000-25000/= mto wa shepu ya soseji 30,000/- zote zikiwa na foronya

Mashuka mashuka. karibuni kuna mdau wangu aliniomba sana sana mashuka. haya kazi kwako ila sijaleta pic nyingi, ni foronya 2, shuka 1, duvet cover 1, tshs. 80,000/=





Hizi zinaitwa writh ni za kutundika mlangoni. tshs. 30,000/=

Kazi ya jumapili. Nilikwenda kumfungia mteja mapazia niliyomtengenezea. ASANTE MAMA CATHERINE WA MBEZI. Wewe wangoja nini?

Jumapili ya jana tarehe 20/12/09 nilikwenda mbezi ya kimara kwenda kumfungia mapazia mteja wangu Mama Catherine. kwa kweli nashukuru kazi yangu ameipenda. Aliniomba nim dizainie mapazia ya sitting room kwake na jikoni. Nikaenda kwake kuangalia anarangi gani na dizaini za furniture alizonazo. Sasa nilimchagulia matirio ya vitambaa na nikamuonyesha akapenda. Nika dizaini mwenyewe, na nimechagua dizaini hii ya mapazia kwa sababu makochi yake tayari yana urembo. Hivyo ningeweka urembo mwingine kwenye mapazia pasinge onekana. Guess what, X-MASS TREE AMEPAMBA MTOTO WAKE WA MIAKA 6 AMBAYE NDIE CATHERINE AKISAIDIWA NA DADA YAKE MLEZI. NILIUPENDA SANA MTI. NINACHOTAKA KUSEMA MTI WA X-MASS HAUNA FOMULA.




Mapazia haya ya kijani ni ya jikoni, nimeamua kuweka kijani kwa sababu kijani inaashiria uoto wa asili, vyakula etc. Kwa upande wa jikoni kama una rangi nyeupe ukutani weka pazia lenye rangi rangi ili kuongeza fleva jikoni na kupunguza ukali wa rangi nyeupe.
Picha za chini ni kabla sijaweka curtains

ujambo sisy merry x-mass & happy new year to Shamim aka. Zeze From Mrs. Jossanne-New York





nawatakia afya njema uzima, wewe na familia yako, na marafiki zako na zaidi new year & new resolutions welcome to the gym shammy ha ha ha ha ha ha upo hapo nitakkta kwenye hizo tred mill nakutakia mafanikio, mema, chaooooo koku NY.

(Kumbe na kwenye mazoezi uko eheheeee!!! thant's very good, haya ngoja na mie nijipange sasa dada- from Sylvia Kreative Homez-Homes Deco)

upangaji wa bafuni, au maliwatoni

Jamani sio kila kitu kinakaa kwenye dressing table, mimi sina mengi ya kusema, Mrs. Jossanne ameshaongelea, na umejionea ukihifadhi vitu kwa usafi na mpangilio basi na nyumba,ofisi etc. kutakuwa kusafi. Tueite Kreative Homez (Homez deco) na tutakusaidia. (Sylvia - Homez deco) She is Cute is she?


Wakina mama, wakina dada, wakina baba usafi ni kitu cha muhimu sana, especially linapokuja
la bafuni na kwenye vyoo tunavyovitumai viwe vya kukaa, au kuchuchumaa, lazima usafi upewe kipaumbele iwe nyumbani, ofisini, kiwandani hospitalini, mashuleni, madukani, usafi usafi ni jambo ambalo baadhi ya watu hawajali vyoo kuwa visafi au bafu.

Ikumbukwe kwamba magonjwa ya maambukizi, magonjwa ya zinaa yanaanzia huku, Nijukumu la kila mmoja make sure sehemu unayojisitiri ni safi, maji unayotumia makopo munayotumia vyooni, yawe masafi siku zote kuna vijidudu ambavyo havionekani kwa macho ni hatari sana,
hasa kwa sisi wakina mama, wakina dada lazima tuwafundishwe, watoto, kunawa mikono, kila mara, una toilet ya kawaida iwe safi, weka dettol kwenye maji kill bacterias.

Wakina mama, wakina dada ni reseach nyingi sana zimefanyika kuhusu kansa ya mlango wa kizazi mara nyingi ni uchafu, hata ktk nchi zilizoendelea, kwa suala la usafi ni la kwetu wote si la DC, AU RC SERIKALI ZA MITAA, UNA JIRANI MCHAFU MWAMBIE TUACHE KUONEANA AIBU, WENYE NYUMBA AMBAO HAWANA, VYOO VYAO VIMEJAA WARIPOTIWE MARA MOJA, USIPANGE NYUMBA AMBAYO INA MATATIZO YA VYOO, MABAFU, NAWATAKIA X-MASS NJEMA WOTE, mzingatie hayo tutakuwa tukielimisha ktk makala mbalimbali, asanteni.

UPANGAJI WA MASHUKA MATAULO, FORONYA NK



NADHANI upangaji wa vitu nilivyovitaja vyumbani makabatini, kama una mpango wa kujenga nyumba yako au kununua , unaweza kufanya, marekebisho, ukaweka kabati la kujengea, ukutani au ukanunua, special stand, ukapanga mashuka taulo, kuanzia ndogo kubwa, foronya za mito kama una baadhi ya mabegi makubwa unakuwa na sehemu yake, pia kwenye closet, nitazidi kuwaelimisha, msiwe na hofu kuuliza, hii yote ni kusadiana tusiwe wachoyo unajua kitu unakaa kimya,uwaambie wenzio hatutafika kwa mpango hu.

Wenzetu wamepiga hatua za maendeleo ktk nyanja mbalimbali kwa kuelimishana kukosoana, siyo kashifa wala majigambo, nawatakia x-mas njema.

HIZO NI CLOSETS AU MAKABATI YA NGUO. Nyumbani kwa Mrs. Jossanne George




Wapendwa lazima tuzingatie upangaji wa nguo hasa kwa wale ambao wamejengea makabati ukutani, au hata una kabati lililojengewa, una kabati la kawaida la nguo panga nguo kufuatana na rangi tuepukane na jungle closets, rainbow colors nguo ziendane na rangi.

Hand bags, mikanda, viatu, mi binafsi nafanya hizi kazi huku kipindi hichi cha baridi tunaenda majumbani tunaorganise vitu mbalimbali, wezangu wao wana campany yao mi naenda kujifunza, tusiwe wavivu wa kujifunza, kila jambo be coachable, be ambitious, tuwe na kiu ya kujifunza kila tunapoenda, sehemu,wanawake wenzangu tusikalie kitu kimoja weee.

Maana wengi wa kina mama, wakina dada, kila kitu tunamwachia dada nyumbani afanye hii big dont, muonyeshe mfano dada, watoto, wako, ndugu zako, kwa muda kidogo unaoupata,

Huna muda kuna wenye uzoefu kama dada Sylvia watakusadia upangaji wa vitu ndani ya nyumba msiwe wabahili, usafi ,upambaji. Upangaji wa vitu ni garama, garamikia uishi ktk mzingira masafi tuzingatie sana rangi kuna rangi ambazo zinaendana na kuna ambazo kamwe aziendani hata kidogo, so uliza kuuliza si ujinga ni kuelimika.

Mama zangu, dada zangu, bibi zangu, hata baba zangu, na wengineo woote nawatakia merry x-mass from:

MRS KOKU JOSSYANNE GEORGE NY.