Thursday, June 28, 2012

Site mbezi......Homez Deco, tuliweka pazia......

 Nyumba ikiwa bado haijawekwa pazia.........
 Mafundi wakitoa pazia, na mwingine aki drill kwa ajili ya kuweka chuma za pazia,
 Chuma zimewekwa, na tunaanza kuweka pazia sasa.....
 Nikikagua kazi......

Tayari pazia zimewekwa..... Kwa kweli pazia hupendezesha sana nyumba, kama mnavyojionea.........Design hii ya pazia ni Eyelet.......

Wednesday, June 27, 2012

Uzinduzi wa Rangi za Dulux za kampuni ya Sadolin Paints..


 Nilipata picha ya pamoja Kutoka Kushoto, Vailet, Mimi, Mr. Geoffrey yeye ni Protective Coating Manager, na Renalda, tukiwa na zawadi zetu.......
 Ukuta umepigwa rangi na tuliohudhuria.......

 Nilialikwa na Mr. Ilyas, yeye ni Sales Manager .........
 Mlango ulipigwa vanish........
 Nilivyoona hii picha kwa kusema ukweli, nilimkumbuka Jaydan wangu, enzi hizo.... tutakavyokimbizana kwa utundu.... hahahhahha hahhahha..... hahhahah


 Rangi za milango/mbao zipo pia........unang'aa mlangooooo kama kioo..........hahhahahah nice.....

 Kulikua na fashion show ya watoto walituandalia.....




 Nilipenda huu mchoro..........


 Kuta zao kwa nje ya madarasa, wamechora picha za Tinga Tinga.... zinavutia sana,......si unaona ni kama wamebandika... kwa jinsi zilivyopendeza......

 Huu mti sio wallpaper, umechorwa kutumia rangi zao, na umependeza kweli.... hongera kwa mchoraji.....kwa kazi nzuri....
 Tulipata fursa ya kupaka rangi kwenye moja ya kuta waliyotuandalia..... na watoto......

Ilikua ni jumamosi ya wiki iliyokwisha, nilialikwa kwenye uzinduzi huu, na siku ilipofika nikawasili hapo. Shughuli ilifanyika katika kituo cha kulelea watoto cha SOS.....

Rangi hizo mnazoziona nje ya majengo ndizo za DULUX za kampuni ya SADOLIN Paints.... najua wengi wetu tunaifahamu kampuni hii ya Sadolin...

Uzinduzi wa rangi hizi mgeni rasmi alikua Mheshimiwa mama Salma Kikwete.  Mheshimiwa mama Mary Nagu pia alikuwepo, na wengineo....

Shughuli ilikua nzuri, na ilienda vizuri, na tulipewa nafasi ya kujaribu rangi hizo kupaka ukutani na kujionea wenyewe...

Kwa kusema ukweli rangi hizi za DULUX ni nzuri, na ziko rangi za kila aina unazozitaka, kutokea kwenye rangi zilizo pooza, mpaka zile kali.....(from neutral colors, cool colors, warm colors etc.....)

Ninapenda kuchukua fursa hii kwa kushukuru kualikwa na kujionea mwenyewe..... na nimealikwa kiwandani, kwenda kujua zaidi ya hizi rangi, na kupata maelezo zaidi juu yake..

Ninawaahidi kuwaletea yote nitakayokua nimeyapata kutoka kwao...........

Bila kusahau nilipewa zawadi......... unataka kujua ni zawadi gani hiyooooo.......

Endelea kua nasi......

NB:

Niliwaahidi mwaka huu na kuendelea, mungu akitupa uhai, nitawaletea vitu vizuri, vya kuboresha ujenzi wa nyumba/ofisi zetu....... na kuremba nyumba kisasa.........Kazi imeanza sasa..........








Tuesday, June 26, 2012

Site Makongo......

 Homez deco tuliweka curtain poles.... vyumbani, nilipenda na vingine.....
 Nilipenda design ya makabati ya jikoni, na jiko lake ni dogo, lakini ameli design na limependeza sana... simple and neat.........top ya makabati ni marble.... hapa wengi tunachanganya sana kati ya marble na formaica,
 Ninashauri kwa jikoni, tutumie mbao, makabati na top ziwe ni marble.... maana sikuhizi kuna hizi mdf, zinazotengenezea makabati, jamani zile hazitaki maji kabisaaaaaa... sasa ukiweka jikoni na jikoni kuna maji,,,, utakuja kuniambia.....na mbao nchini kwetu tunazo, na mafundi wako, na nitajitahidi kuwaletea contact za mafundi pindi ninapopata, na kuona kazi zao nikaridhika nazo,
 Niipenda pia nyumba kwa nje... nyumba haijahamiwa bado, na ni juu na chini, yaani ni familia mbili watakaa hapa..... Nzuri sana na imependeza.....hii design ya madirisha kwa nje, naona ndio iko kwenye fashion sasa, nyumba nyingi inazo, na inavutia....
 Hii ni corridor, nilipenda hizo nguzo, natafuta contacts zao nitawapa, soon,
 Bafu....
 Toilet..... Tiles ziko nyingi na za aina tofauti, na ubora tofauti, sasa ni wewe tuu chaguo lako , na jinsi ya kuzipangilia ziweze kuendana, nzuri sana.....

Kwa haraka tuu nilivyoingia ndani ya hii nyumba nilijua tuu mwenye hii nyumba anapenda sana neutral colors......

Nashukuru sana kwa mwenye nyumba kwa kunipa ruhusa na contacts za mafundi ili sisi sote tuweze kupendezesha nyumba zetu,

Na ninaamini kwa kufanya hivi, mafundi feki watajichuja tu wenyewe.....

Namba ya fundi ni 0753-218817

NB:
Mafundi hawa, sijaonana nao, ingawa ninatafuta muda nionane nao, niendapo site, nikipendezewa na kazi zao basi ndio ninaomba contacts, kwa wenye nyumba..... Ninawashukuru wote wenye nyumba kwa ushirikiano wao.....na tuendelee na moyo huu wa upendo..........





Wednesday, June 20, 2012

Site ya Kigamboni....


Sink kama linavyoonekana hapa juuu...napenda kushauri kua kwenye sinks, muweke kabati, kwani inakusaidia sana kuhifadhi vitu vya bafuni na kukaonekana kusafi muda wote, vitu kama toiet paper, sabuni za vyooni etc....

Bafu hiloooooo....

Jiko nalo haliko nyuma kabisaaa.....unajua ukijiamini n kujua unapenda nini, na kufuatilia majarida mbali mbali, ama kwenye mitandao, basi unaweza...decorate nyumba yako na ikapendeza.... pia....wenye nyumba hawa waliamua kusafiri wenyewe, kufuata mzigo, yaani kuanzia, grill, miango, jiko, tiles etc, china na wanasema waliokoa pesa kwa kiasi kikubwa tuuu.....

Hii ndio nguzo ilivyonakshiwa......na nilichopenda, layer yake ni kubwa, yaani hawajabania kabisaaa........


Hii ukutani sio tiles, ni design ambayo wataalamu wanachanganya ndio wanaweka ukutani, ukiingalia kwa karibu, ni kama undongo hivi.......imekaa vizuri kweli yaani....

Nilivutiwa na nyumba hii nilivyofika, kwani ukiangalia ukuta kwa nje umependeza, kwa design yake, ukiangalia kwa taratibu utaona jinsi nguzo zilivyonakshiwa......
kwa watakaohitaji huduma hii ninawaletea contacts zake kesho mapema......
Hongereni sana wenye nyumba, na ninashukuru sana kwa kunikubalia kupiga picha na kuja kushare na wadau wenzetu, ili wajue ni wapi wapate vitu vizuri...
NB:
Ninawaomba wadau wote kua kama unajua kuna mahali vitu vinapatikana vya majumbani, iwe ni mapambo, vitu vya ujenzi, naomba usisite kuniambia, unipe contacts zao halafu nitawatafuta na kuwasiliana nao, na kuwaletea nini wanafanya, na ninaomba ushirikiano wenu ninapoomba kupiga picha nyumba zenu, ili kuja kushirikiana na wadau wenzetu, naomba mnikubalie, kwani sitotaja majina ya mwenye nyumba, ama details zozote zitakazofanya kujulikana kua nyumba hiyo ni ya nani kwa upande wetu....ninajitolea kufanya kazi hii bila malipo yoyote.

Asanteni sana, na mungu awabariki.....

Tuesday, June 19, 2012

Kabati za ndani.... Mbao aina ya mninga....mbao zetu....










Jumapili ya juzi, nilikwenda site eneo la Goba....., lengo ni kwenda kupima pazia, na hii ni baada ya sisi kuweka curtain poles, kama kawaida yangu, jamani kizuri kisifie.....na chema chajiuza....
Nyumba hii ni nzuri, na nilipenda na nikamsifia sana mwenye nyumba, na ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kuniruhusu kupiga picha ili tuweze kushirikiana katika hili...
kuna msemo usemao, kizuri kula na nduguyo, na kibaya ........
Nilipenda kila kitu, yaani tiles, makabati etc.....
Nimeonelea tuangalie makabati haya na uniambie kua umeyaonaje,
kwa mtazamo wangu, fundi aliyeyatengeneza haya makabati anastahili sifa, maana haku chakachua, na finnishing yake ni nzuri. maana hata milango pia ni mninga......na fundi huyu hana usumbufu wa kazi.......
kwa mahitaji ya milango makabati wasiliana na fundi huyu
anaitwa fundi Dennis - 0715 - 888680
Ninamshukuru tena mteja wangu huyu kwa kutupa mawasiliano ya huyu fundi ili wote tusingie hasara, maana mafundi asilimia kubwa ni kula hela za watu na kiswahili kingi....