HD blog is proudly sponsored by Dulux Paints(Sadolin)

Thursday, May 23, 2013

Kifuatacho......(80% ni maandalizi 20% kupaka rangi)


Homez Deco tulipata kazi ya kupiga rangi nyumba iliyoko maeneo ya kinondoni......Rangi ya nyumba nzima ilikua ni cream......
 Hapa ni nyumba ikipigwa msasa mlaini, nikiwa nina maana ya tunafanya maandalizi ya ukuta. Ukipiga msasa mlaini ni unaondoa rangi iliyochoka na uchakavu wowote uliojificha......Hatua hii mara nyingi mafundi hua wanaikwepa na kulipua kazi na matokeo yake kazi inakua chafu.......(20% maandalizi ya ukuta 80% kupaka rangi)
 Mafundi wakiendelea na kazi ya msasa kwa ajili ya matayarisho......rangi tulipiga sitting room, dinning, na korido.....ilituchukua siku mbili kumaliza kazi...mafundi walikua ni 3. Kutayarisha ukuta ilituchukua siku moja nanusu.......na tulifanya kazi kuanzia asubuhi mpaka saa tatu usiku siku ya kwanza. na siku ya pili tulimaliza saa moja jioni.....




Hili ni vumbi la rangi iliyochoka baada ya kupiga msasa mlaini nyumba hii.......

Tutaende kuleta picha zaidi......

Tuesday, May 21, 2013

Rangi bora na imara kwenye nyumba/ofisi yako......

Rangi ni nini?
Rangi ni koti ya kukinga ama kulinda..(it's a protective coating)

Rangi imetengenezwa kutokana na mchanganyiko wa malighafi., na inaweza kupakwa kwa kutumia brashi, rola au kwa kupuliza, na itakapo kauka inakamata ama kushikana vizuri na sehemu uliyoipakana hivyo kupendezesha na kukinga sehemu hiyo.......

Sasa basi rangi sio tuu hupendezesha kuta zetu bali hata kukinga.......

Ukiangalia mchoro wetu hapo chini utaona ni jinsi gani rangi inakua na mchanganyiko mpaka kuitwa rangi.....

  • Malighafi
  • viendelezi
  • Gundi
  • Viyeyushi
  • Viongezo
 Mchoro wetu hapa chini unaonyesha jinsi ya utengenezaji wa rangi unavyopaswa kuwa......
 Sasa kazi iko hapa kwenye picha ya chini....Tofauti ya utengenezwaji wa rangi......
Katika picha ya kwanza huu ndio utengenezwaji unaostahili wa rangi, na ndipo unapopata rangi imara na yenye mvuto na kuvutia yaani inavigezo vyote vinavyostahili......

Thursday, May 16, 2013

Unafanyaje vibaraza vya nyumba yako maji yanapotuama na kuweka ukungu?





Tumekua tukisumbuka sana na tatizo la vibaraza vya mbele ya nyumba zetu, kuharibiwa na mvua, ama hali ya unyevu unyevu kipindi cha baridi.....kutokana na maji kutuama kutoka kwenye paa na kuja kwenye vibaraza vya nyumba zetu...

Na mara nyingi tumekua tukipata suluhisho la muda ambalo ni mvua zinapomalizika tunapaka rangi.

Sasa ningependa kuwajulisha kua suluhisho tunalo katika tatizo hili....Katika kampuni ya
Dulux wametuletea suluhisho ambalo ni product inaitwa RAINSHIELD.

Rainshield ni aina ya rangi ambayo, hairuhusu maji kupenya, nikiwa nina maana kua yenyewe inaruhusu maji kuteleza na sio kutuama (water resistant, crack resistant and it's long lasting acrylic formulation). Product hii husaidia sana katika sehemu za nje kama vibaraza......

Inapatikana katika rangi nyeupe na kijivu isiyokoza....

Lita 1 inatumika 2-3 square meters kutegemea na ukuta ulivyotayarishwa.

Zinapatikana katika ujazo wa lita 5.





Wasiliana nasi......0713 - 920565. karibu.

Tuesday, May 14, 2013

Suluhisho la kwenye ukuta unaosumbuliwa na fangasi, unyevu unyevu, etc.....




 Kuna kuta ambazo zinasumbuliwa sana na fangasi ama unyevu unyevu, sehemu hizi ni kwenye njia za mabomba, sehemu uliyoweka air condition, nje sehemu ya garden inayozunguka nyumba etc.....

Huu ndio muonekano wa tatizo la fangasi ama maji yavyoharibu ukuta......



Kwa mtazamo wa hizi picha utakubaliana nami kua hili tatizo lipo katika baadhi ya nyumba zetu.....matatizo haya ni kua yanaletwa na  maji ya ardhini kupanda juuu etc.....jamani wakati wa kuanza ujenzi, nikiwa namaana msingi ukisha chimbwa ni muhimu kuweka pvc plastics...... Hizi ni plastics zinazoweka layer ya maji ama unyevu unyevu kugusana na tofali...na hivyo kufanya nyumba kua imara.

Sasa kuna baadhi ya nyumba hua hawaweki....ama kwa kutokujua, ama kwa kukwepa gharama.
Kuna msemo usemao KUNA MAKOSA YANAYOSABABISHWA NA FUNDI MJENZI....HIVYO FUNDI RANGI HAWEZI KUYAMALIZA BALI HUYAGHAIRISHA KWA MUDA NA SI KUYAMALIZA......

Kwa mfano hili swala la kuta kuwa na maji maji, ama unyevu unyevu.....asilimia kubwa ni kwamba hazikuwekwa pvc wakati zinajengwa na hili ni kosa la fundi mjenzi....sasa akija fundi rangi hato tatua tatizo bali atalighairisha kwa kutumia products za kuzuia Unyevu unyevu ama fangasi ......na baada ya miaka kadhaa litarudi tena.....

Tatizo lingine ni kutokana na rangi zenyewe. kuna baadhi ya rangi hua zinaleta fangasi kwenye kuta za nyumba zetu....hili nitakuja kuliezea pia......


 Hizi ni kuta kwa nje
 Hapo juu ni ukuta kwa ndani.....
Ukuta kwa nje.....



Product hii ya DAMP SHIELD. ni product mahususi kwa matatizo kama haya.......

Kwanza kabla ya kutumia hakikisha unatayarisha ukuta wako vizuri na kwa kutibu tatizo...mfano, kama mabomba yanavuja basi hakikisha umelitengeneza kwanza ndio utumie hii damp shield..... halafu suribia ikauke vizuri, piga msasa,  futa vumbi na ndio upake rangi yako uliyokusudia......

Product hii inasaidia maji kuto haribu ukuta wako kwa 50%.......na hali hizo ambazo nimeziongelea hapo juu.


Karibuni sana Homez Deco maana mkombozi amepatikana.......

Maelezo....
  • Inakauka baada ya masaa 2 baada ya kuipaka mahali husika.
  • kuirudia kuipaka ni baada ya masaa 4.
  • 12 square meter katika lita moja.....upakaji wake ukutani.
  • Rangi yake ni nyeupe...
Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa email: sylvianamoyo@yahoo.com  Tel: 0713 - 920-565

Monday, May 13, 2013

Matayarisho/Maandalizi sahihi ya ukuta kabla ya kupaka rangi.....( iwe ni kuta za ofisini ama nyumba zetu).......


Somo letu linaendea........na leo tunaangalia upande wa matayarisho ya ukuta kabla ya kupaka rangi......

Kuna msemo usemao: DAIMA SAFISHA NA PAKA RANGI...... NA SIO PAKA RANGI NA USAFISHE.

Sasa sisi tunageuza na tunatumia: PAKA RANGI NA USAFISHE.....

Msemo huu Daima safisha na paka rangi maana yake ni kua, katika matayarisho ya ukuta kwa ajili ya kupaka rangi, tunahitajika kutumia 80% katika kutayarisha ukuta, na 20% ndio kupaka rangi......

Ila sisi ama wengi wetu tumekua tukitumia 20% Kutayarisha ukuta na 80% ndio kupaka rangi....kitu ambacho ni makosa makubwa mno....na hii ni kutokana  na ama fundi hajui, ama mwenye nyumba ana haraka ya nyumba kuisha, ama mwenye nyumba anakwepa gharama, ama fundi amedanganya na kupotea na hela....na sababu nyingi nyingi......

Hawa ni baadhi ya maadui wa rangi katika ile 80% ya kuandaa ukuta:


  • Kabla ya kupaka rangi yoyote ile kwenye ukuta, hakikisha sehemu hiyo iko katika hali ya kuridhisha, nikiwa na maana kua kuna maadui wa rangi ambao ni vumbi (kuta zenye vumbi mfano wa chokaa...kama gypsum powder ni mfano wa chokaa), oil, grisi, kutu, mchanganyiko wa kemikali, unyevu, na fangasi ama vimelea vya wadudu.
  • 80% ya malalamiko ya kuhusu rangi yanatokana na maandalizi duni ama yasiyo sahihi ya ukuta, kwenye usafi, kuziba matundu, kuondoa rangi iliyobanduka na isiyokamata vizuri, kutoondolewa kwa ukungu na fangasi, kutokusafisha vizuri kuta zenye chokaa, ama kutondoa rangi ya zamani na varnish etc.....



Hapo chini tunaoneshwa kua hayo ndio maandalizi ya ukuta ambayo tumeyazoea na tumekua tukiendelea nayo. 

  • Njia ya kwanza tuliyoizoea baada ya kujenga nyumba hua tunapiga ripu.(ripu ni mchanganyiko cement na mchanga).
  • Pili, tunafanya skimming kwa kutumia white cement na rangi ya maji unachanganya, na wengine wanatumia niru, na wengine ndio hiyo gypsum powder wanachanganya na maji.
  • Tatu, ikishakauka tunapiga msasa.
  • Nne, kufuta vumbi ukuta wako uliopiga msasa.
  • Tano, Kupaka primer.
  • Sita, tunapaka under coat.
  • Mwisho ni kupaka rangi yako iliyokusudiwa....
NB:
Sado binder (primer) ni gundi ambayo huhitajika kupakwa baada ya kuvufuta vumbi ukuta wako....husaidia rangi kushikana na ukuta,.....rangi hua haishiki kwenye ukuta wenye vumbi ama sehemu yenye vumbi ndio maana hubanduka.....sasa kwa wale waliotumia gypsum powder ama white cement hii sado binder itawahusu mnoooo.......

Picha hii hapo chini ndio ukuta livyozoea kuuandaa...


(kwenye picha hii hapa juu maneno yasiyoonekana ndio hayo hapo chini.

UKUTA LAZIMA UWE MSAFINA MKAVU USLEWENAVUMBI, UCHAFU, OILI AU GRI.

TUMIA KITU SAHIHI CHA KUSAFISHIA KAMA KUNA ULAZIMA

BRASHI SKRAPA AU MSASA KUTEGEWEANA NA KITU, MFANO MBAP CHUMA CHENYE KUTU. MDIA KWENYE PLASTA

ZIBA MATUNDU AU NYUFA. ANGALIA KIWANGO CHA JOTO NA UNYEVU (KAMA INTUFAYIKA)







Kwa kawaida ukuta unatakiwa kua na unene wa microns (thickness) 125 kama hapo juu inavyoonekana katika mchoro wetu.....Mchoro wetu huu unaeelezea kua tumechukua karatasi ndio kama ukuta wetu......na tukapaka primer ambapo ina 20 microns, tukaongezea undercoat ambapo ni 45 microns na mwisho tukapaka coat mbili za rangi tuliyokusudia kupaka ambapo kila coat ina microns 30 . hivyo basi tunapata microns 125 ambazo ndio zinahitajika katika ukuta wako ziweko......

Katika hapa sasa, ili kulinda ukuta wako, hautakiwi na sio vizuri kupunguza ama kuzidisha......maana italeta madhara hapo siku za baadae....Nikisema kuzidisha ama kupunguza ni kwamba, baadhi ya mafundi hua wanaongeza maji mengi kupiliza kwenye rangi na rangi kua ni nyepesi zaidi nikiwa na maana inawezekana hawajui makadirio, ama wanabana matumizi ...ama mteja unaibiwa bila kujijua......


IFUATAYO NDIO MAANDALIZI SAHIHI YA UKUTA WAKO WA NYUMBA AMA OFISI:
  • Kama inavyoonekana hii ni Smoothover skimming plaster, kazi yake ni kufanya skimming ya ndani na nje ya nyumba yako.....na product hii hutumika mara baada tuu ya kupiga ripu nyumba yako..... 
  • Baada ya kupaka utahitajika kusubiria ikauke na ndio upige msasa ukuta wako.
  • Utahitajika kufuta vumbi.
  • Na mwisho ndio upake rangi yako uliyokusudia.......
Smooth over inapatikana katika ujazo wa
 1.5 kg
35 kg

matumizi yake ni 1 square meter = 1 kg(smooth over skimming plaster lakini pia inategemea na unene,  unaoupaka ukutani)

kwa hiyo hakuna haja ya kutumia white cement, ama gypsum powder kwa ajili ya skimming na wala huhitaji prima ama under coat.....SMOOTH OVER SKIMMING PLASTER INA COVER EACH AND EVERYTHING.......

Kwa mahitaji yako ya Smoothover wasiliana nasi Homez Deco kwa simu 0713 - 920565 ama email: sylvianamoyo@yahoo.com

Karibuni sana....