Thursday, February 2, 2012

Kazi ya Homez Deco.........Hii ni restaurant iko njia panda ya africana mbezi, mwisho wa ukuta wa mbezi tiles

 Muonekano wa nje wa restaurant......kumbuka barabara inajengwa, ndio maana wakaweka daraja la muda hapo.......
 Hawa ni wafanyakazi wa The Junction Restaurant....... Unajua bwana mi nimempenda mmliki wake, kwa kuchagua wanawake zaidi, mwanaume ni mmoja hakuwepo siku hiyo..... Sio siri nilifurahi sana kua wanawake wanapewa kipaumbele kwenye kazi....ona walivyo wasafi,, na mpishi anaonekana, waitress anaonekana, manager anaonekana........Hongera Elly.......Hapauzwi pombe......
 Nilikaribishwa na juice kwanza, yaani hapa wateja wote ni sawa, si mnajua kua akienda mwanamke, haudumiwi haraka, akienda mwanaume ndio huduma fastaaaa. hapa hakuna hiyoooooo  Niliipenda hii juice, jamani ni nzito kama vile wana shamba la matunda......
 haya  counter hiyoooooo kusafi kweli kweli......
 dada yuko bize,,, na ni wasafi hawa atu wa jikoni,, hivi si unajua kwenye hizi restaurant zetu, jamani ni wachafu... utadhani chakula kikitoka hapo ni cha 5 star hotel duh...
 Jiko........ hakuna mainzi hapo..... maana niliingia kila kona.......
 mlango wa kuelekea toilet....

 I was happy.....kwa kazi zao walivyojipanga.....
 kusafijeeeee,,,,..... Hongera Elly....
 Haya jiko hilooooooo.................. walikua wanafanya matayarisho ya chakula cha mchana...
 toilets.......
 I love my self........



Hii picha naipenda sanaaaaa,,,, sasa basi Elly yeye anapenda sana timu ya manchester, sasa basi nilichofanya nikapaka hiyo rangi nyekundu, na nikachanganya na zinazoendana, ili kuipooza hiyo red, na ukiangalia hiyo picha ndio kabisaaaa inazidi kuvutia.....
 

Haya kwa wale wenye sehemu za biashara, karibu tuwasiliane, sio lazima eti iwe ni biashara kuubwa, hata ndogo uliyonayo, tuta decorate, kumbuka kwamba, kwenye biashara kinachomvuta mtu wa nje ni rangi.........

Karibu The Junction Restaurant......

No comments:

Post a Comment