Thursday, July 18, 2013

Public Toilets and Bathrooms....

Umeshawahi kukutana na toilet ambapo ukipita kwenye korido, unasikia harufu mbaya inatoka na kusambaa korido nzima, ama kama tena na hiyo toilet iko karibu na sitting room ama dining room basi ndio harufu yote inasambaa................

Kumekua na tabia kwa asilimia kubwa, watu kudharau ama kuona kinyaa kufanya usafi kwenye vyoo....vya nyumba zao...ama kumuachia tuu msichana wa kazi afanye usafi ajuavyo bila kumfuatilia usafi umefanyika vizuri tena kwa dawa zinazotakiwa kutumika, maana utakuta ukuta una ukungu ama kutu , masinki nayo basi vurugu tuuuuuu.......


Baadhi ya toilets/bathrooms.....na asilimia kubwa yakwetu hua hatuweki hizi glass ambazo hua zinazuia maji kurukia kwenye toilets seats...




Asilimia kubwa ya huku kwetu siku hizi hua tunaweka tiles ukuta mzima wa toilet zetu, kitu ambacho ni kizuri na kinapendeza...pale tuu kama hizi tiles zime mechishwa vizuri kwa wale wanaoweka tiles za urembo. Kwa wale wanaoweka tiles za rangi moja nyeupe pia hupendeza..

Tatizo linakuja kwenye usafi. je usafi unafanyika mpaka kule juu, ama ndio unafanya usafi pale unapofikia tuu....

Maana kwenye kuoga lazima maji yatarukia ukutani, na kuacha madoa madoa ya uchafu. Jamani hua inaleta kinyaa pale unapoingia na kutaka kuoga ama kufanya shughuli zako zingine halafu unakuta toilet ni kuchafu...halafu ukizingatia ni  nyumbani kwako.......maana siku hizi hata vyoo vya kulipia ni visafi muda woteee.

Nina mshukuru sana MAMA  yangu kwakua alinifundisha usafi tokea mapema...kuna msemo usemao, mkunje samaki angali mbichi......

Professional ya Mama yangu ni Housekeer, na ana experience ya 17- 18yrs ya hotel na sasa ni mwalimu wa Housekeeping & Laundry katika chuo cha Taifa....u can emagine inakuaje nyumbani.....

Yaani ilikua ukiingia tuu toilet, haijalishi unafanya nini, ni lazima uhakikishe unaacha toilet safi, na kavu muda wote. Ukiwa unakwenda kuoga, basi hakikisha ukitoka ukuta ni mkavu, na chini kukavu, na sink la toilet ni kavu muda wote....

Na ile tabia ya unaingia kuoga, unalowesha, towels, ama toilet paper, alikua haipendi.... yaani akikuangalia tuu, unajua kasema nini...maana saa ingine alikua haongei anakutizama, mwenyewe unarekebisha kosa lako.......

Tena hata kama hauingii kuoga ama etc....toilets/bathroom zinachekiwa muda wote........sio eti mpaka uwende haja......

Ilikua hakuna cha msichana wa kazi ama mtoto wake...wote mnafanya kazi kama kawaida hakuna kuleana kizembe....maana mwisho wa siku na mtoto unakuja kua na nyumba yako mama hatokuwepo.

Hii husaidia sana kua kusafi.

Maana kwa upande wa hotels, kuna wale wanaofanya usafi katika public areas, kama ume notice ama umeona, hua mara kwa mara wanaingia toilets na kuangalia usafi na maeneo yote ya reception, etc.....na ndio maana tunaona hotels muda wote ni kusafi.

Ukiweka utaratibu huu wa kila mara kuangalia kama vyoo nivisafi, na kila anaeingia anahakikisha amekuacha ni kusafi, na kwa upande wa kufanya usafi unafanya usafi mpaka  juu ya tiles...na kutumia products nzuri za usafi na kuua vijidudu, na kuweka maua yanayotoa harufu nzuri, ama sprays etc za kuleta harufu nzuri. Nakuhakikishia sehemu hii itakaa safi, na kukavu kila muda.

Baadhi ya products za usafi:

 Hizi ni baadhi ya products za usafi ninazozifahamu, na hazina kemikali, na matumizi yake ni wewe ndio unapanga maana una dikute wewe mwenyewe kulingana na matumizi yako...


Kwa mahitaji ya products hizi wasiliana na 0754-006977 anaitwa Tija........na atakupa maelezo zaidi.

1 comment:

  1. hi Sylvia, hzo glass zakuzuia maji yasiloweshe choo zinauzwa wapi? Nazitafuta sana zijazipata

    ReplyDelete