Wednesday, July 31, 2013

Ukarabati wa vyumba vyetu katika kipindi hiki cha kuelekea kusherehekea sikukuu.............

Tumeshazungumzia, sebule, dinning, korido, vyooni na sasa tunaelekea vyumbani na kisha tutakuja jikoni, na nje ya nyumba zetu.......

Katika eneo hili la chumbani, hapa ni mahali pa kupumzika, ama kulala unapohitaji, kama ni usiku ama mchana.......Mwili unahitaji kupumzika, na kama unahitaji kupumzika, basi hakuna budi chumba kiwe kisafi, kizuri, na kiwe na nafasi....

Hivi mi jamani hua ninashangaa kwakweli, kuona vyumba vimejaa vitu. na kama mnavyojua vyumba vyetu vya kulala hua ni standard size....kama ndio 12 by 12 ama 10 by 10....kama ni nyumba ya kupanga ama ni nyumba yako.......sasa kwanini mtu usiweke vitu ambavyo utavitumia, na kuliko kurundika vitu?

Kwa mfano, unakuta mtu kaweka kitanda 6 by 6, makabati , dressing table, shoe rack, stand ya pochi, na tv, kochi, hanger ya nguo etc......basi ni kurundika vitu tuuu

Cha msingi jamani kwanza angalia ukubwa wa chumba chako, na ikiwezekana ukipime kama hujui size yake....na baada ya hapo, weka vitu kulingana na ukubwa wa chumba......sasa utakuta chumba ni kidogo lakini mtu anaweka kitanda kikubwa ama kabati kubwa.....yote haya ni ya nini?

Na huko kwenye makabati kuna nguo nyingi mtu na zingine hazivaliki......yaani kabati mpaka linalemewa....sasa ukija kwenye viatu ni vingi mno, na vingine huvai labda kwa kuharibika, ama umevichoka....ila bado unavyo tuuuuu....

Naomba kushauri kua vitu ambavyo hutumii jamani GAWA......

Kwa kufanya hivi itakusaidia kupata nafasi na hewa izunguke katika chumba chako, kua na vitu vingi sio kupendezesha nyumba........

Kwani ukiweka vitu kulingana na chumba chako, tena kwa mpangilio kutakua na tatizo?

Kwa upande wa rangi za vyumbani, tafadhali rangi zipakwe zilizopoa, maana rangi nazo zinachangia kwa kiasi kikubwa mno katika kukufanya u relax.....

katika vyumba vyetu tukumbuke pia usafi wa kina, ukianzia usafi wa cyling board, madisha, mashuka...etc.....

Dressing table zetu jamani hua tunazisahau.......mafuta yakidondokea hua yanaacha alama, vitana navyo....etc

Rangi hizo baadhi ni.................
 Kama rangi ina kiza, basi ipakwe kwenye upande mmoja wa ukuta na  kuta zingine ziwe na rangi ambazo ziko angaavu...



Pazia nazo ni muhimu, katika vyumba vyetu, sebule, dinning, jikoni etc........

Kitanda ni utandikaji wako wewe mwenyewe, labda kiwe na mito mingi, ama mashuka 2 ama duvet etc....ni wewe tuu upendavyo,

Bila kusahau taa za chumbani, zisiwe na mwanga mkali mno.....waweza kuweka shades ili kupunguza mwanga, hii husaidia chumba kiongezeke mvuto zaidi pale itakavyofika usiku........

No comments:

Post a Comment