Monday, July 8, 2013

KUPAMBA KITANDA KWA KUTUMIA MITO.......

 Mandhali ya chumba chako cha kulala ni wewe ndie unae amua kiweje, na kipendeze vipi......Hapa leo tutazungumzia jinsi ya kupamba kwa kutumia mito.....Katika upambaji wa aina hii kwanza kabisa hakuna kanuni ya uweke mito mingapi katika kitanda chako.....ni idadi unayoitaka wewe...kulingana na ukubwa wa kitanda chako.....Mashuka pia yanachangia kwa kiasi kikubwa mno kupendezesha chumba chako......

 Siku hizi mashuka asilimia kubwa yanauzwa yakiwa na foronya nne na kuendelea......sasa ni wewe tuu mwenyewe unataka kitanda chako kiweje.........mfano kwenye kitanda hiki kuna mito 8. na size ya kitanda hiki ni n5 by 6, ambapo shuka/duvet hili lina foronya mbili, nikiwa nina maana mashuka huja na foronya zinazofanana na mashuka ndio maana unaweza kujua kua lina foronya ngapi....

Sasa hizi foronya zingine unahitajika kua mtundu kidogo, ili uweze kuchanganyia.....mito ya nyuma ni off white, rangi hii huendana na rangi yoyote ile, mito mingine ndio hii rangi ya mbele ambayo maroon, na ukiangalia kwenye shuka iko foronya hizi huja na mashuka uliyonunua, na ile rangi ya off white imejirudia tena... na mto wa mwisho umejirudia kwa rangi ya maroon na ua la off white.....na imependeza....kwa muendelezo huu sio lazima ukanunua kila kitu sehemu moja, nikiwa na maana sio sehemu nyingi wanakua na foronya za ku mechishia...waweza tembea tembea na kuulizia na kupata maduka ambapo utapata foronya hizo za ku mechishia....
Kwenye vitanda vyetu hivi hivi pia ukweka bed runner, hupendeza mno.....yaweza kua ni rangi zinazoendana ama zinazokaribiana  angalau,.......mfano ni huu hapa kua, kuna bed runner ya chui chui, halafu ikawekwa ya maroon kwa juu yake......na muonekano unazidi kuvutiwa kwa kuongezewa mito kwenye kiti cha kuvalia viatu, ile chui chui imejirudia, halafu maroon, na brown ambayo imetoka kwenye rangi za chui chui....

Nahapa hata ingetumika papo pia ingependeza...maana unachukua rangi za kwenye mashuka yako ndio muongozo wako katika upambaji wa kitanda chako......

Namna hii nakuambia unapumzisha mwili wako vizuri baada ya mihangaiko siku nzima na kuamka ukiwa na nguvu tele na mawazo mapya kwa siku inayofuata....

Upambajio wa nyumba yako unaanza na wewe mwenyewe, na sio mtu wa nje....ukishaa amua ndio mtu wa nje anaweza kukusaidia....

Homez Deco tunakukaribisha kwa maswali, maoni, ushauri, na hata huduma zetu katika hili na mengineyo mengi....Karibuni....

NB:
Homez Deco tutakusaidia kwa kiasi kikubwa kukutafutia foronya za ziada kwa ajili ya kumechishia mashuka yako....wasiliana nasi: 0713 - 920565

No comments:

Post a Comment