Tuesday, July 16, 2013

KORIDO ZA NYUMBA ZETU....


Naomba leo tuangalie upande wa korido, baada ya kua tumeshaona sitting room, dinning room........

Katika eneo hili, kwa upande wa kuanzia usafi na rangi ni muhimu sana kuzingatia
Korido nyingi hua hakuna dirisha ama madirisha...hivyo kunakua na kiza cha aina flan hivi.......kulingana na ulivyojenga.

Hapa kuna nyumba aina mbili: kuna ambazo ni fupi na kuna ambazo ni ndefu (urefu kutoka juu mpaka chini).......ingawa wengi wetu tunajitahidi kujenga nyumba ndefu kulingana na maendeleo na mabadiliko ya kila kukicha.

Mtakubaliana nami kua kwenye korido zetu hua zinachafuka mno, maana utakuta mtu akipita mwingine kashika na mikono yake michafu, ama mwengine anashika tuuu basi ilimradi tabu tupu, na hivyo kufanya korido kuchafuka, na kama ndio haukua umepaka hizi rangi za wash 'n' ware ama silk maana rangi za aina hizi hua unaweza kusafisha na maji na uchafu ukapungua ama kuisha kulingana na uchafu wenyewe.

Kama unaona ukuta wako hauridhishi, basi waweza kupaka rangi, kwa kuuandaa ukuta wako. Mwite mtaalam, akupe hesabu ya rangi inaingia kiasi gani na gharama zake na aina ya rangi.......hivyo atauandaa ukuta kwa kupiga msasa, na kuziba mashimo kama yako, nashauri mtumie skimming plaster smoothover za dulux, halafu apake rangi iliyokusudiwa kama ni za Dulux etc.......

Rangi za korido ni light colors, ama rangi zenye mwangaza......Kumbuka katika eneo hili hakuna madirisha hivyo mwanga kupenya ni asilimia ndogo mno, ni nyumba chache zenye madirisha katika eneo hili.

Sasa unapopaka rangi zenye kiza, korido inakua ni ndogo, na giza na haitakua na mvuto wowote, hata kama kuna taa ambazo utaziwasha wakati wa usiku.......

Baadhi ya rangi za kupaka korido ni hizi, ingawa inategemea pia na sitting room na dinning room umepaka rangi gani......





Hizi pia unaweza ukahitaji ziwe light zaidi....na zikafaaa pia.....ama kama zilivyo.....

Mara nyingi hua ninashauri ukitumia mtaalam ina kua ni rahisi kukuhauri ni rangi ipi itapendeza kulingana na ukubwa ama udogo wa korido yako......

Ukipaka rangi yenye kiza kwenye korido yako, itafanya kua ni ndogo zaidi na yenye kiza........ona rangi hizi na uone jinsi zilivyo  dark halafu upake kwenye korido yako:


Tunakaribisha maswali, na tunatoa ushauri pia....Karibuni


No comments:

Post a Comment