Thursday, May 10, 2012

Homez Deco Website........(Suprise......)


Napenda kuchukua nafasi hii, kwa kuwashukuru wadau wangu wote kwa support yenu,
Leo ni siku yangu rasmi nakuja kwenu kuwaeleza kua tumefungua website yetu... Tunawaomba comments zenu, za ushauri wowote ule kwa jinsi mtakavyo iona kama tubadilishe nini, iweje ili iweze kua nzuri na ya kuvutia, ama hivyo ilivyo inatosha
Sasa basi,
Website hii iko pamoja na blogsite, blog itaendelea kuwepo, ila ukiingia kwenye blogsite kama tulivyozoea hutoweza kuona changes, ila ukiingia kwa address hii hapa chini utaona changes, na kuna vingi vipo, na vinaendelea kuwepo kutokana na mahitaji yenu.........,
kingine ni kwamba website yetu hii iko tofauti kidogo, kwani utaweza ku Scroll up & Down, topics, na matangazo yakawa pale pale.........ama kama tulivyo zoea ukatumia ya pembeni......
Nina furaha sana sanaaa, maana ukimya wangu ni ilikua kwa ajili ya website hii yangu iweze kuwa tayari mwanzoni mwa mwezi huu kama nilivyo ahidi....Mungu ni mwema na namshukuru kwa kila jambo...
Kuazia sasa Mtakua mkiingia kwa kupitia address hii: http://www.homezdeco.co.tz
Karibuni......

2 comments:

  1. Sylvia dear, hongera sana jamani.

    Yaaaani nimefurahi sana nilipoona your new website, manake nimekuwa nachungulia huku mara kumi kumi kujua surprise ni nini, teh teh

    Dadangu, yaaani napenda sana kazi yako na jinsi unavyokazana kupambana na maisha, kweli unaniinspire sana. Kila la heri dada

    Najiandaa vizuri na nitawasiliana nawe kwenye kuboresha nyumbani kwangu.

    ReplyDelete
  2. Hard work always pays. mungu aibariki kazi ya mikono yako. much love

    ReplyDelete