Thursday, February 28, 2013

SOLD...

  Price tshs. 200,000/- kitanda pamoja na godoro. Size 6 by 6
Kitanda kimeuzwa......
 Price tshs. 45,000/- office drawer. Kimeuzwa...
Price tshs. 15,000/- Kimeuzwa...


Vitu hivi vina umri wa miezi 6 tuuu

NB:
Naomba kwa maswali yote muwasiliane na namba ya simu niliyoweka hapo juu......yeye ndio atakaye weza kuwapa majibu ya maswali yote muulizayo......

Tuesday, February 26, 2013

SOLD

 Price tshs. 60,000/-(Stand ya kuanikia nguo)
 Price tshs. 35,000/-(Stand ya mbao ya pochi. makoti) Imeuzwa

Monday, February 25, 2013

Kitchen Hood.....

Hili ni jiko la mdau wetu.....ambapo Homez Deco tulimpakia rangi za Dulux...Lakini pia nilivutiwa na jiko lake.  Mnakumbuka kuna siku katika blog yetu nilizungumzia kuhusu Kitchen Hood, na kazi yake.....Kazi yake ni kunyonya unyevu na mvuke ambao hua unachafua sana jiko.....
Nilipendezewa pia na jinsi alivyo weka lebo katika kontena zake za kuhifadhia chakula...Kama inavyoonekana hapa.....Hata siku moja haitaweza kukupa shida ya kuanza kutafuta kontena ipi ina nini.......maana unaweza ukawa una kontena nyingi na zikakuchanganya...

Hili pia nililizungumzia la kuweka lebo kontena za chakula. na zinatakiwa ziwe zinazoonyesha ndani kuna nini.....
Mimi binafsi nilipendezewa na jiko lake,

Napenda kuchukua fursa hii kukupongeza mdau wetu, kwa kua na jiko zuri na safi na lakisasa.....

(nitaomba contacts za hawa waliotengeneza jiko hili ili wadau nao muweze kua na majiko ya kisasa kama hili, maana finishing yao ni nzuri mno)

Nitalipiga picha jiko zima na kuweza kuwaletea humu humu.......

Friday, February 22, 2013

For Sale items....


Habari wadau,

Baada ya ukimya kidogo kwenye blog, ambao ni kwa ajili ya kazi, za kwenda site......

Leo ninakuja kwenu na mada ya kuuza vitu vya ndani ambavyo hamvitumii, ama mnataka kubadilisha, mtoe vya zamani mlete vipya...

 Iwe ni majumbani ama ofisini, iwe ni vya garden ama garage

Sasa basi vitu hivi mnaviweka wapi? ama mnafanya navyo nini?

Huku ninakotembea, hili swala ninakutana nalo, naniongea na wadau, na ninashukuru kwamba wanaliitikia, na naona tunaanza kutoa vitu vyetu na kuviuza, kwa bei ambayo ni reasonable, na hata wewe muuzaji utapata hela ya kufanyia kitu kingine.....

Utakuta vitu ni viko katika hali nzuri mtu kavijaza ndani, ama kaweka stoo, ili mradi tuu ni vurugu....nyumba imejaa, hakuna nafasi, vitu vimesongamana....na bado analeta vingine...

Hivi unajua kua kabla ya kwenda kununua kitu lazima ukitafutie sehemu ya kukaa kwanza ndio ukanunue....

Nawaomba watanzania wenzangu, kwenye suala la ku pamba nyumba zetu hili nalo lipo.....la kupunguza vitu ndani, kabla ya ku anza kupamba.....Vitu vingi vikijaa ni uchafu, nasio kwamba ndio nyumba imekua ya kisasa.....kwa kujaza vitu.....

Chochote ulichonacho, na ambacho haukitumii...tuko sisi tunaweza kukitumia ni wewe kuamua kukitoa....

Homez Deco tumejitolea kukusaidia kuviuza vitu vyako kwa kutanga kwenye blog yetu, na wadau wavione na waweze kununua. kwa watakaohitaji...

Kuliko kukaa na kitu, mpaka kinaharibikia stoo.....na kuendelea kueleta msongamano wa vitu ndani...

Vitu hivi vinaweza kua ni fanicha yoyote ile, iwe ni ya ofisini ama nyumbani...

Na visiwe vimechoka sanaaaa ama vimechakaa sana......viwe katika hali nzuri....maana Homez Deco kabla ya kuviweka kwenye blog ni lazima tuviangalie...

Utahitajika kututumia picha ya kila upande  wa kitu hicho unachotaka kukiuza....

Zoezi hili ni kwa yoyote yule...iwe ni Dar ama mikoani.....



Tuwasiliane kwa email; sylvianamoyo@yahoo.com ama simu: 0713 - 920565.....


Thursday, February 14, 2013

To all my fans







Vinapatikana Homez Deco.....viko tayari

 Magazine racks

Stand ya pochi ama makoti etc.....

Vitu vyote hivi kila kimoja bei ni tshs. 65,000/-

Wallpaper ziko kwenye Sale......

 Wallpaper ziko kwenye sale roller moja ni tshs. 80,000/-

Wednesday, February 13, 2013

SOLD......Frem ya kitanda inauzwa...size 5 by 6....Bei inanzia 200,000/- bei inapungua......


 Frem ya kitanda kwa mbele....(kitanda hiki kinauzwa na mdau mwenzetu....anabadilisha fanicha za chumbani....) Na hii ni katika muendelezo wa kuuza fanicha zetu...badala ya kuvifundika ndani....tunakukaribisha uweze kuvitangaza humu katika blog yetu......
 Frem ya kitanda kwa pembeni...
Frem ya kitanda kwa nyuma.....

Umri wa kitanda hiki ni mwaka na nusu.......bado kiko katika hali nzuri.....

Kwa mahitaji ya kitanda hiki wasiliana nasi 0713 - 920565, email sylvianamoyo@yahoo.com

TUNAKUKARIBISHA KUTANGAZA NASI KATIKA KUUZA FANICHA ZAKO ZA NDANI AMA ZA OFISI AMA ZA GARDEN....KARIBUNI.....

Elegant Wood Works.......

 Hii ni kampuni inayoshughulika na fanicha za mbao, zikiwemo, milango, madirisha etc.....

Tuesday, February 12, 2013

Hii ilikua ni birthday ya Jaydan ametimiza miaka 2. Tarehe 8/2/2013...Ilifanyika Mary Brown ya masaki....siku ya jumapili tarehe 10/2/2013

 Huyu ndie Jaydan wangu....Birthday Boy...2yrs sasa......
 Mama na mwana.....
 Nilitinga kivazi hiki.......
 Mama na mwana kabla ya party kuanza....
 Jaydan akiwa na kaka yake nje ya mary brown kwenye michezo....
 A kiss from my son......





 Michezo ilianza na watoto walicheza na kufurahi......yaani kama birthday boy Jaydan...alicheza karibu michezo yote.....alichangamka kupita maelezo....sasa nikajiuliza kwani amejua kama ni sherehe yake ama ni uchangamfu tuu.....hahhahahha nilifurahi sana sana....
 Baby girl anaitwa Nuru, na wamepishana mwezi mmoja na Jaydan wangu.... hapa akiwa kwenye pozi.....
 My best friend Halima.......marafiki wa kweli ni kwenye shida na raha.......thanks dear......
 Baby girl yeye alitulia akiwa anangalia wenzie wakicheza.....
 Dada yangu, wa tatu kutoka kulia.......akiwa na rafiki, na ndugu na jamaa.....( asante mama mkubwa kwa support)
 Dada wa mary brown akiandaa mshumaa kwa kuwasha...
 Cake....Nilichagua cake ya winnie the pooh......kwa mtoto wangu......
 Jaydan katika pozi....


 Halima na binamu yangu.....na watoto...
 Ulifika muda wa kukata keki.....


 Tulimuimbia wimbo wa happy birthday.....(akawa anashangaa shangaa mwenyewe) hapa najua hakuna aliye hisi, maana machozi yalikua yananilenga lenga.....sikujua hali hii ilitokea wapi...ila nilijikaza kuto toa chozi.....na shughuli iweze kuendelea......Thanks Lord aliniweza kuto dondosha chozi....
 Hapa akizima mshumaa.....alizima mwenye...alipuliza mara tatu na ukazimika...nilicheka mwenyewe tuuu
 Nilimsaidia Jaydan kukata keki....
 Nilimlisha Jaydan wangu keki yake......na kum busu shavuni......this moment i will never forget......I love you my son....
 Haya ikafika zamu ya mama kulishwa keki......ila hapa tulipata kazi kidogo....maana kila ukimpa anilishe...akawa anakula kwanza yeye....baadae ndio zoezi liliendelea la kulishana......hhahahhahah...
 Kaka Tevin akilishwa...ni mtoto wa dada yangu.....
 Huyu ndie dada yangu...nae alilishwa keki.....
 Huyu ni dada yake Jaydan....yaani namshukuru Mungu kila siku kwa kunipa huyu dada...niko nae tokea najifungua Jaydan.....na ananitunzia mtoto wangu vizuri...namshukuru dada.....sana sana......
 Keki zikiendelea kulishwa kwa watoto wengine.....


 Ulifika muda wa chakula......na kila mtoto akawa busy na chakula chake....
 Anaitwa Jamson, yuko na mama yake....
 Jaydan kwenye msosi akiwa na dada yake.....
 Hapo tumeshakula, sasa tunasoma ramani tuanzie wapi kucheza,,,,,,
 Dada yangu na rafiki yangu Haneem....Thanks for coming dear....

 Nikiwa na rafiki yangu Halima.....kwenye pozi la camera.....hahahhahah
 Rafiki yangu Haneem...


Nikiwa katika pozi tofauti tofauti........

Namshukuru Mungu kwa kila jambo na kuweza kunipa nguvu, uvumilivu, amani ya moyo, na kuweza kunikuzia mwanangu.....

Mwakani Jaydan ataanza shule, hivyo naendelea kumuomba mungu aendelea kunipigania, na kunipa nguvu na uhai, niweze kumlea Jaydan wangu vizuri, na kua mwenye utiifu, na mwerevu etc......


NB:

Napenda kuwaomba radhi kwa ukimya uliojitokea wa kuto upload blog kwa sababu zilizo nje ya uwezo wangu............ila sasa nimerudi....Nawashukuru kwa uvumilivu wenu......Asanteni.