Wednesday, November 20, 2013

FORONYA ZINAPATIKANA HOMEZ DECO........MATERIALS KUTOKA UK NA UTURUKI.....KARIBUNI......


 Size ya foronya hizi ni 45 by 45 na mito pia inapatikana. Mito hubadilisha muonekano wa makochi yako na hupendezesha......
 bei ya kila foronya ni 12, 000.










Monday, November 18, 2013

KAZI YA KUWEKA TILES NYUMBA IKO KIBAHA......

 Homez deco umepata kazi katika nyumba hii iliyoko kibaha ya finnishing ya nyumba nzima mpaka ikamilike.
 Tuliaanza kwa kufanya window shopping na mteja ya tiles katika maduka na tukaipata hii design ambapo wote tulikubaliana tuiweke hii aina ya tiles kwa ushauri wangu.
 Ukiangalia kwa mbali hatujaweka scarting maana tutaweka ya mbao nyunba nzima.

Saturday, November 16, 2013

SOFA SET INAUZWA...............INA MWEZI MMOJA TUU TOKEA INUNULIWE.....NI MPYA KABISAAAAAAA


 Sofa hii inauzwa kwa bei ya 2,900,000/-    ilinunuliwa Orca Deco, sasa anaeuza kwa bahati nzuri anahamishwa kikazi nje ya nchi........sofa iko katika hali nzuri kama inavyoonekana...na tokea ainunue amekaa nayo mwezi mmoja tuuuu.Color ni Dark brown, purple na cream....

Wednesday, November 13, 2013

FINNISHING YA NYUMBA ZETU........



Wengi wetu tumekua tukidhani kua kazi nzito ni ujenzi wa nyumba na sio finnishing,,,,naomba kuwaeleza leo kua sio kweli kwa asilimia flani........

Jamani finnishing ya nyumba ni gharama kuliko ujenzi....tutambue hilo, na utakuta wengine mpaka miaka kadhaa hawajamaliza, kwa kua wanajua nini wanafanya ...

Kinachohitajika ni kujipanga, na kutafuta mtaalam aweze kukusaidia katika hili....unaweza kujenga nyumba yako vizuri...lakini ukija kwenye finnishing unaanza kubania hela na kutaka virahisi...yaani jua kua nyumba unaiharibu na hutokua umefanya kazi yoyote ile......nyumba itakua mbaya mbaya na unaweza kujuta.....


Tujitahidi katika hili kua kama najenga nyumba yangu basi ni afadhali nifanye taratibu kwa ufasaha kuliko haaraka haraka na ukaharibu kazi......

Tujitahidi kua wavumilivu katika kumaliza nyumba zetu kuliko haraka haraka, ninasema hivyo kwa kua nakutana na watu kama hawa, na kwa kweli katika kazi yangu sipendi haraka ya kupitiliza kabisaaaaa.......

Kazi ya designing inahitaji muda na nafasi. bila hivyo ni kuharibu kazi.....nami sipendi hilo litokeeee....

Kwa kwetu Tanzania bado tuko nyuma katika hili ingawa tunajikongoja na tutafika kwa kuelimishana na kuelewana...

GRILLS DESIGN......

 Tunayo furaha kuwatangazia kua tumeanza kutengeneza grills za madirisha na milango.  Hizi ni baadhi ya designs tulizonazo, na tutaendelea kuwaletea designs nyingi kadri tuwezavyo......

TUNAOMBA JIBU LA SWALI LAKE KWA MDAU MWENZETU........

Naomba mnisaidie jinsi ya kuosha madumu( vyombo) vya kuhifazia maji, nimetumia njia mbali mbali but naona bado ile rangi ya kijani imekataa kutoka, yanaoneka machafu kweli coz ni meupe na mkono haupenyi ndani..
thanx, mdau wa Arusha.



Monday, November 11, 2013

KWA WALE WOTE WENYE WATOTO WATUNDU WANAOCHORA MAKOCHI........RANGI ZINAZOFAA ZA MAKOCHI.....

 Habari za muda kidogo wadau wangu, nilikua kimya kutokana na majukumu ya kifamilia kidogo, na sasa tuko sawa.

Sawa, sasa kuna tatizo kidogo, kwenye uchaguzi wa makochi ya kwenye nyumba zetu, kwa wenye familia ya watoto wadogo, kwanza kabisa ninachoweza kusema ni kua mtoto ukimfundisha anaelewa, na ukimdekeza atakupa hasara..........sasa ni wewe tuu uamuzi wako.......

Nimekutana na tatizo hili la makochi kuchorwa chorwa na watoto wetu, na jamani bei za makochi tunazijua zilivyo gharama........na pia kwa kua tuna watoto basi hatuna budi kununua makochi ambayo rangi zake ni dark na sio light.......kupunguza tatizo la watoto wetu kuchora kwenye makochi yetu.....

Hebu fikiria umenunua kochi lako kama ndio off white ama cream then likachorwa chorwa na mtoto, kama ni cartoons ama ndio anajifunzia homework etc......

JIBU KWA MDAU







Naomba kumjibu mdau wangu aliyekua ananiuliza kua hii meza ipo.na jibu ni kua meza ipo, na imebaki moja tuuu.....bei ni 1,250,000/=

Karibu tuwasiliane, na samahani kwa kuchelewa kukujibu kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu.





Monday, November 4, 2013